KWA ANAYETAKA KUOA NASHAURI USIOE MWANAMKE MWENYE SIFA HIZI

Nina miaka 20 kwenye ndoa hivyo nina uzoefu wa kutosha na nimeona mengi kwenye maisha ya ndoa . 


Nimeona ndo zilizodumu na ambazo zimevunjika ndani ya muda mfupi. Katika maisha ya ndoa kuna mivutano mingi tu ila kuna ambayo inavumilika na mingine isiyovumilika. Ila ukioa mwanamke wa status fulani basi chances kubwa za kushindwana huko mbeleni zinakuwepo.

 Mimi nilioa miaka 20 iliyopita nikiwa na umri wa miaka 26 na mke wangu akiwa na 22. Tulikutana wote tukiwa na maisha ya kawaida though mimi nilikuwa university graduate na mwenzangu ni high school graduate but she was business talented. 

Hakuna ambae alikuwa na mtoto wala kuoa au kuolewa kabla but we are now blessed with three kids. We are noT reach yet lakini tunaishi kwetu, tunabiashara zetu, tunaishi maisha mazuri na watoto wanasoma shule nzuri ila tulianza kuishi maisha ya chumba kimoja cha kupanga. Ushauri wangu unajikita kwa kijana anaetaka kuolewa hivyo mwengine anaetaka kushauri anaweza kujikita kwa msichana anaetaka kuolewa.


Kwanza kabisa mwanaume ana nafasi kubwa sana ya kudumisha ndoa yake na ndoa kuvunjika sehemu kubwa sana weakness inakuwa upande wa mwanamme. Sababu inaweza kuwa makosa uliyofanya wakati wa kuchagua mchumba au maisha baada ya kuoa. Sifa za mwanamke nitakazotaja inaweza ikaonekana namnyanyapaa mwanamke la hasha ni kwamba tu nataka tuwe realistic mambo yanayoleta mifarakano kwenye maisha ya ndoa. Here we go




1. Usioe mwanamke aliekuzidi umri. Wenzetu umri wao unaonekana unakwenda kwa kasi sana bila kujali ana matunzo ya aina gani. Hivyo basi mwanamke uliempita miaka mitano huko mbeleni yeye atakuwa mzee kuliko sasa je kama yeye kakupita umri je huoni utamchoka mapema sana?


2. Gap kati ya mwanaume na mwanamke isizidi miaka kumi ili ku maintain swala la kumtosheleza mwenza wako lifetime kulingana na umri wenu. Wanaume tukisha anza miaka 55 kuelekea 60 ukweli ni kwamba nguvu nazo zinaanza kupungua sasa kama umepishana umri mrefu na mke kubali kwamba utasaidiwa


3. Mwanamke mwenye mtoto. Kubali tusikubali hili nalo ni tatizo kubwa sana kwanza kwa kijana unakwaza wazazi wako. Kwanini uwaanzishie wazazi wako na wajukuu wakambo? Sawa umempenda mke wako japo ana mtoto lakini huoni kwamba mke ni wako sawa ila umeleta kwenye jamii yenu hivyo ni vizuri na wazazi na ndugu zako wakafurahia mtu asie na doa. Kwani vijana mnakosea wapi mbona wachumba bado wengi tu. Hapa siongelei case ya mjanae kukutana na mgane au Divorcee kukutana na Divorcee these could get married but a fresh young chap.

4. Mwanamke uliompora toka kwa mwanamme mwengine sababu ya pressure fulani either mwanamme alikuwa hana hela ukamzidi, either mwanamme alikuwa ameoa already, either mwanamme alienda kusoma. Kumbuka wanawake ni watu wenye huruma na kukumbuka sana. Ukioa mwanamke wa aina hii ataendelea kumriwadha huyo jamaa yake siku zote if the man would be interested. Lakini wewe pia utakuwa na kazi ya kumchunga huyo mke wako siku zote ili asije akakutana na ex wake. Hapa ndio maisha ya wivu kwa kwenda mbele kama nyie mnaishi Arusha na Ex anaishi Dar mama akisafiri kuelekea Dar na wewe unataka kwenda. Na ni kweli akienda kama wakifanikiwa kukutana watakulana tu.

Comments